Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Biashara Wafugaji watupia Ma-DC zigo la migogoro hifadhini
Biashara

Wafugaji watupia Ma-DC zigo la migogoro hifadhini

Spread the love

MWENYEKITI wa Chama Cha Wafugaji Tanzania (CCWT) kimesema wakuu wa wilaya wanachangia kwa sehemu migororo ya wafugaji kwa kuchochea ukamatwaji wa mifugo pindi inapoingia kwenye mbuga za hifadhi ya serikali. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma… (endelea).

Hayo yamelezwa Jijini Dodoma leo Jumatatu na Mwenyekiti wa CCWT Taifa, Mrida Mshote Marocho katika mkutano mkuu wa uzinduzi wa kadi za kielekroniki kwa wanachama wa chama hicho.

Kaimu Katibu mkuu na Mkurugenzi wa huduma za mifugo, Prof. Heziron Nonga (wa kwanza kushoto) akishuhudia Mwenyekiti wa Chama Cha Wafungaji Tanzania (CCWT), Mrida Marocha (kulia) na Kaimu meneja Kanda ya kati Dodoma (CRDB) Andrew Mheziwa (kushoto) wakati wakisaini makubaliano ya haki kati ya pande zote mbili kwa ajili ya mikopo ya asilimia tisa yaliyofanyika jana kwenye mkutano mkuu wa wafungaji uliofanyika Dodoma

Mwenyekiti huyo amesema kutokana na uwepo mgogoro kati ya wafugaji na wakuu wilaya, Serikali inaombwa kuona namna bora ya kuwakutanisha wafugaji na wakuu wa wilaya ili kutatua migogoro pale mifugo inapoingia kwenye hifadhi.

Pamoja na mambo mambo mengine ameiomba serikali kuona namna bora ya kutenga na kuboresha maeneo ya malisho ya mifugo sambamba na uboreshaji wa majosho ya kuoshea mifugo.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mwenyekiti amesema wafugaji wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusumbuliwa kwa ukamatwaji wa mifugo yao.

Amesema hivi karibuni ng’ombe zaidi ya 100 zinashikiliwa na mkuu wa wilaya tunduru mkoamni Ruvuma ahali inayosababisha usumbufu kutokana na kile kinachosadikiwa ni kuingia katika maeneo ya hifadhi.

Katika hatua nyingine kiongozi huyo wa wafugaji amewataka wanachama wa chama hicho kujiandikisha kwa kutumia kadi za kielekroniki ili kuepukana na kutapeliwa.

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa chama hicho, Busundwa Wamarwa amesema wafugaji wafikirie uwekezaji katika viwanda kwa ajili ya kuongeza thamani ya mifugo yao.

Amesema maeneo mengi ya ufugaji yanakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa maji hivyo jambo ambalo ameeleza kutokana na hali hiyo wafugaji wamekuwa wakijikuta wanahamahama.

Pia amesema wafugaji wanatakiwa kuwa na umoja na ufugaji wenye tija na uboreshaji wa maeneo ya malisho na sehemu za unyweshaji wa mifugo.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Naibu Katibu mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Ezron Nonnga amesema kwa sasa serikali imeshanunua mizani 70 kwa ajili ya kupima uzito wa mifugo.

Amesema kuwa utaratibu ambao kwa sasa umewekwa na Serikali ni kuhakikisha mifugo inauzwa kwa thamani ya uzito na siyo kuuzwa kwa makadirio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Meridianbet yatoa msaada Mwenge

Spread the love  KAMPUNI ya Meridianbet imefika maeneo ya Mwenge jijini Dar-es-salaam...

Biashara

Serengeti yakabidhi mkwanja kwa mshindi wa Maokoto ndani ya Kizibo

Spread the love Mshindi wa Maokoto ndani ya kizibo kutoka Kahama Mjini...

Biashara

Ushindi rahisi unpatikana kila ukicheza kasino ya Hot Joker

Spread the love  HOT Joker Fruits 20 ni mchezo wa sloti ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Zara tours yajivunia kupandisha wageni 228 Mlima Kilimanjaro

Spread the loveKampuni ya utalii ya Zara tours ya mjini Moshi mkoani...

error: Content is protected !!