Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yamkabidhi majukumu Spika Tulia kuhusu IPU
Habari za SiasaTangulizi

Serikali yamkabidhi majukumu Spika Tulia kuhusu IPU

Spika Dk. Tulia Ackson
Spread the love

SERIKALI imemtaka Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dk. Tulia Ackson, kutumia nafasi hiyo kuhakikisha analinda maslahi ya Tanzania katika jumuiya za kimataifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Maagizo hayo yametolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, leo tarehe 30 Oktoba 2023, katika hafla ya kumpokea Dk. Tulia ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tanzania, iliyofanyika jijini Dodoma.

Waziri Majaliwa amesema, Serikali ina mikataba mingi iliyoingia katika Umoja wa Mataifa, hivyo inaamini Spika Tulia atatumia nafasi hiyo kupenyeza ajenda za Tanzania.

“Sisi tumefarijika kama Serikali, sababu moja kati ya majukumu yako kwamba utakuwa unahudhuria vikao vyote vya Umoja wa Mataifa na sote tunajua kwamba Serikali yetu tunayo mikataba yetu tuliyokuwa nayo kwenye Umoja wa mataifa,”

“ Sisi tunashukuru sababu tutakutumia utakapokuwa unaenda kwenye vikao kwa kuingiza ajenda za nchi. Tuna hakika utatupigania,” amesema Waziri Majaliwa.

Katika hatua nyingine, Waziri Majaliwa amesema viongozi wa nchi wanampongeza Spika Tulia kwa kushinda nafasi hiyo nyeti, akisema ameiheshimisha nchi  na mhimili anaouongoza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!