SERIKALI imesema ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu jumla ya watumishi wa umma 190,781 wamepandishwa vyeo baada ya kusubiri kwa muda mrefu licha ya kuwa na sifa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Hayo yameelezwa jana Jumatano tarehe 16 2022 na Waziri wa Ofisi Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Jenista Mhagama, akielezea mafanikio ya mwaka mmoja wa Rais Samia madarakani.
Mhagama amesema upandishwaji huo wa vyeo na madaraja umeigharimu Serikali jumla Sh 39 bilioni ndani ya mwaka mmoja.
Aidha, amesema ndani ya mwaka mmoja Rais Samia amelipa malimbikizo ya mishahara kwa watumishi 65,394 ya jumla ya Sh 91.8 bilioni, “ni maamuzi ya kijasiri, maamuzi ya busara na ya kuonyesha namna gani Rais wetu anawapenda watumishi wake.”
Vilevile amesema Rais Samia aliamua kuwabadilisha kada watumishi 19,386 na ubadilishaji huo uligharimu Sh 1.3 bilioni, “ndani ya mwaka mmoja akatekeleza jambo hili la kishujaa kabisa.”
Leave a comment