Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watatu wafariki dunia Kilwa kwa kula kasa
Habari MchanganyikoTangulizi

Watatu wafariki dunia Kilwa kwa kula kasa

Spread the love

WATU watatu akiwemo mtoto mwenye umri wa mwezi mmoja wakazi wa kijiji cha Rushungi wilayani Kilwa mkoani Lindi wamefariki dunia baada ya kula samaki aina ya Kasa-ng’amba ambaye aliokotwa ufukweni mwa bahari. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Lindi jana tarehe 10 Oktoba, 2022, Mganga Mkuu mkoa huo, Dk. Kheri Kagya amesema tarehe 5 Oktoba, 2022 Zahanati ya Rushungi iliwapokea watu waliokula samaki huyo wakiwa na matatizo ya kuhara, kulegea mwili na wengine kupoteza fahamu na mtoto mmoja alifariki katika zahanati hiyo.

Dk. Kagya amesema hadi kufikia asubuhi tarehe 9 Oktoba, 2022 watu waliofika zahanati ya Rushungi walikuwa 33 na kati ya hao 13 walipewa rufaa kwenda kituo cha afya Kitomanga manispaa ya Lindi.

Amesema baadae watu watatu ambao ni wanaume hali zao zilikuwa mbaya zaidi na kupewa rufaa hadi hospitali ya Mkoa wa Lindi, Sokoine.

Ameongeza kuwa watu hao watatu waliopewa rufaa kwenda Sokoine, wawili wamefariki dunia ambao ni mwanaume mwenye umri wa miaka 41 na mtoto mwenye umri wa miaka 8 huku mmoja akiendelea na matibabu katika chumba cha uangalizi maalum.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!