Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watanzania 940,000 wapata chanjo ya korona, zingine laki 5…
Habari Mchanganyiko

Watanzania 940,000 wapata chanjo ya korona, zingine laki 5…

Rais Samia Suluhu Hassan akichanjwa chanjo ya korona
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imesema, hadi kufikia juzi Ijumaa tarehe 15 Oktoba 2021, takiribani wananchi 940,000 walikuwa wamepata chanjo ya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya korona (UVIKO-19). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Shughuli ya utoaji wa chanjo ilizinduliwa tarehe 28 Julai 2021, Ikulu ya jijini Dar es Salaam na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa yeye mwenyewe kuchanjwa chanjo aina ya Johnson & Jonson.

Leo Jumapilo, tarehe 17 Oktoba 2021, Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa, akitoa taarifa ya wiki ya utendaji wa Serikali akiwa jijini Mwanza amesema, shughuli ya utoaji wa chanjo inaendelea vizuri.

Amesema, Serikali ya Tanzania ilipokea dozi 158,4000 kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), kupitia mpango wake wa kusaidia nchi kupata chanjo.

“Kati ya zile chanjo 158,4000, mpaka sasa Watanzania zaidi kwa takwimu za mpaka juzi zaidi ya 940,000 walikuwa wameshapata chanjo hii. Kwa hivyo kazi inakwenda vizuri,” amesema Msigwa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo

Msigwa amesema chanjo za awamu ya pili zilizoingizwa hivi karibuni, aina ya Sinopharm kutoka nchini China, zimeanza kusambazwa katika halmashauri.

“Tumeshaleta chanjo nyingine dozi 165,000 zimeshafika aina ya Sinofarm kutoka China, tunatoa mara mbili, unachoma matra ya kwanza, kisha ukachome ya pili,” amesema Msigwa.

Msigwa amesema mwishoni mwa Oktoba 2021, Serikali inatarajia kupokea dozi nyingine 500,000 za chanjo ya UVIKO-19, aina ya Pfizer.

Pia, amesema kupitia mpango wa Covax Facility wa WHO, Serikali inatarajia kupata chanjo milioni 12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!