Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Wanne kuiwakilisha Tanzania chaguo la awali Future Face
Michezo

Wanne kuiwakilisha Tanzania chaguo la awali Future Face

Spread the love

 

WANAMITINDO wanne kati ya 200 waliojitokeza kwenye usaili wa Shindano la Future Face 2023 wameteuliwa kuiwakilisha Tanzania kwenye chaguo la awali la Future Face duniani 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Usaili wa shindano hilo la Future Face umefanyika kwa kushirikiana na kuratibiwa na Mwanamitindo wa kimataifa, Millen Happiness Magese jijini Dar es Salaam huku majaji wa nne wakihusika katika kuchuja wanamitindo waliojitokeza hadi kubakia na wawakilishi wanne kati ya hao 200 waliojitokeza.

Majaji katika usaili wa shindano hilo la kimataifa ambalo ndio mara ya kwanza kufanyika nchini Tanzania walikuwa Ally Rehmtullah, Mwanamitindo wa Kimataifa Millen Happiness Magese, Martin Kadinda na Jamilla Vera Swai.

Akitangaza matokeo ya usaili huo Mwanamitindo Magese amesema kuwa vijana zaidi ya 200 walijitokeza kwenye usaili uliofanyika mwishoni mwa wiki.

Amesema baada ya kuangalia sifa na vigezo vya Shindano hilo wamefanikiwa kuwapata wawakilishi wa nne ambao hao watachuana tena na kumpata mmoja ambaye ataiwakilisha nchi ya Tanzania katika mashindano hayo.

Amewataja walioteuliwa kwenye usahili huo ni Rachel Amani Julius(20) – 5’8 Ft, Joyceller Lasway(25l – 5’9 Ft, Neema Evaresty(23) – 5’11 Ft pamoja na Jasinta David Makwabe(25) – 5’11 Ft.

Magese amesema baada ya kupatikana kwa wawakilishi hao hakutakuwa na kambi huku akifafanua yule atakayechaguliwa kuiwakilisha nchi Septemba mwaka huu atakwenda nchini na Nigeria na akifanikiwa kushinda anakwenda nchini Ufaransa au Italia.

“Nawashukuru majaji wote kwa ushiriki na kujitoa kwao kufanikisha jambo hili muhimu ambalo limeandika historia kubwa katika nchi yetu kwani ndio mara ya kwanza Shindano la Future Face linafanyika nchini Tanzania.

” Pia nawashukuru sana vijana wote kwa kujitokeza kwa wingi, sikutegemea kuona umati uliojitokeza na kama mtu hakuweza kufika basi anaruhusiwa kutuma maomba yake kwa njia ya mtandao kupitia www.futurefaceglobal.com ambapo mwisho ni tarehe 22 Septemba 2023″ amesema.

Awali wakati anazungumzia Shindano hilo, Mwanamitindo huyo amesema ameshirikiana na Future Face kuleta Shindano hilo kubwa zaidi la kimataifa la kusaka wanamitindo mwaka wa 2023.

Amesema Shindano hilo ni la kipekee lililoandaliwa na Wakala mkubwa zaidi wa wanamitindo barani Afrika, Beth Model Management na limekuwa na utofauti wake wa ukubwa, umri, rangi na kabila, na ulemavu, huku shindano likiwa na sera ya fursa sawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!