Sunday , 12 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa 60% maeneo kanda ya ziwa hayana maji safi na salama- Mbowe
Habari za Siasa

60% maeneo kanda ya ziwa hayana maji safi na salama- Mbowe

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendelo- CHADEMA, Freeman Mbowe, amesema kuwa zaidi ya asilimia 60 ya maeneo ya ukanda wa Ziwa Victoria, hayana maji safi na salama. Anaripoti Isaya Temu, TURDARco … (endelea).

Jana tarehe 9 Agosti 2023 , Kupitia ukurasa wake rasmi katika mtandao wa kijamii wa X zamani Tweeter, Mbowe amesema maeneo yote waliyozunguka Chama cha Demokrasia na Maendeleo wamekuta yana shida ya maji safi na salama pamoja na kuwa karibu na Ziwa Victoria.

“Maeneo yote ya ukanda wa Ziwa Victoria tuliyopita, zaidi ya asilimia 60 hayana maji safi na salama. Ziwa Victoria linawanufaisha watu wa Misri na nchi nyingine. Geita mjini, Geita vijijini, Nyarugusu, kote huko wana utajiri mkubwa wa dhahabu lakini hawana maji. Wanakunywa maji yasiyo salama yanayochanganyika na madini yenye sumu ya zebaki inayotumika kwenye shughuli za madini,” ameandika Mbowe.

Pia Mwenyekiti huyo cha CHADEMA alieleza shida kubwa inayosababisha ukosefu wa huduma hiyo ya maji Kanda ya Ziwa ni kutokana kuwa na Viongozi wa CCM ambao wameshidwa kuwa na mipango thabiti na kugeuza rasilimali kuwa laana.

“Uongozi mbovu wa CCM umegeuza utajiri mkubwa wa raslimali kuwa a curse of resources (laana ya rasilimali), ameongeza Mbowe

CHADEMA bado kipo maeneo ya kanda ya ziwa kwa ajili ya kufanya mikutano ya hadhara na wananchi kwa ajili ya kutoa elimu kuhusiana na mambo mbalimbali ikiwemo sakata la mkataba wa bandari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!