Watu waliojihami kwa bunduki wamewateka nyara zaidi ya wanafunzi 280 baada ya kuivamia shule moja kaskazini magharibi mwa Nigeria katika mojawapo ya visa vikubwa zaidi vya utekaji nyara kuwahi kushuhudiwa nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa… (endelea).
Maafisa wa serikali katika jimbo la Kaduna wamethibitisha utekaji nyara huo katika shule ya Kuriga hapo jana Alhamisi, ila hawakutoa idadi kamili.
Mmoja wa walimu katika shule hiyo iliyoko mkoa wa Chikun, Sani Abdullah amesema walimu walifanikiwa kutoroka na wanafunzi wengi wakati wavamizi hao walipokuwa wakifyatua risasi hewani.
Mkaazi wa eneo hilo, Mohammad Adam ameliambia shirika la habari la Ufaransa – AFP kwamba, zaidi ya watoto 280 ndio waliotekwa nyara baada ya kufanya hesabu kwa umakini zaidi.
Leave a comment