Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Biashara Wakulima watakiwa kufuata ushauri wa maofisa ugani
Biashara

Wakulima watakiwa kufuata ushauri wa maofisa ugani

Spread the love

MHASIBU wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya kula ya alizeti – Malaika Sunflower Oil, Ester Lumambo amewashauri wakulima wa mazao ya alizeti nchini kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo ili kulima kilimo chenye tija badala ya kulima mazao ya kujikimu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma (endelea).

Lumambo ametoa ushauri huo umetolewa leo tarehe mosi Agosti 2023 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi yanayofanyika kwa mikoa miwili ya Dodoma na Singida katika viwanja vya maonesho Nzuguni Jijini Dodoma.

Amesema wakulima wanatakiwa kulima kilimo ambacho kitawapatia manufaa ya kuingia kwenye soko kwa urahisi na kujipatia kipato kizuri na kuwafanya wanunuzi kununua bidhaa ambazo ni bora na zenye uhakika.

“Sisi ni wafanyabiashara ambao tunanunua mazao ya alizeti kwa wakulima, lakini kuna changamoto ambazo tunakutana nazo kutoka kwa baadhi ya wakulima na changamoto kubwa ni wakulima wanakuwa na mbegu ambazo hazina mafuta mengi.

“Na tatizo hilo linatokana na kukosekana kwa utaalamu mzuri wa kujua ni mbegu gani mkulima anatakiwa kupanda ili waweze kupata mazao mengi na ambayo hayana changamoto yoyote kwenye soko” ameeleza mhasibu huyo.

Aidha, Mhasibu huyo amewahimiza kujenga tabia ya kununua bidhaa ambazo zipo kwenye kiwango cha ubora kwa nia ya kulinda na kutunza afya zao.

Naye mmoja wa washiriki wa maonesho hayo ambaye ni mkulima, kutoka wilaya ya Mpwapwa aliyejitamulisha kwa jina la Levison Lemanya amesema kuwa maonesho hayo yatalenga zaidi kuwaelimisha wakulima ili kulima kilimo chenye tija.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yashiriki maadhimisho Mei Mosi Arusha

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeungana na maelfu ya...

Biashara

Promosheni ya bil 1 kutoka Meridianbet kasino, cheza na ushinde zawadi kubwa

Spread the love  INGIA katika ulimwengu wa zawadi za kushangaza: Jishindie sehemu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

error: Content is protected !!