Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Wabunge waibana Serikali kero ya popo Dar
Habari Mchanganyiko

Wabunge waibana Serikali kero ya popo Dar

Spread the love

WABUNGE wameitaka serikali kuondoa popo waliopo maeneo ya Upanga jijini Dar es Salaam ili kulinda afya za wakazi wa maeneo hayo. Anaripoti Mlelwa Kiwale, TUDARCo…(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya kuwepo na malalamiko kwa wakazi wa maeneo ya Upanga, Sea View, Leaders Club, Kinondoni, Oysterbay, Masaki, Msasani Peninsula na maeneo mengine ya Ukanda wa Pwani kwamba popo hap wamekuwa kero kwa wananchi.

Popo hao wamedaiwa pia kusababisha uharibifu kwa kuvunja vioo vya madirisha kwenye makazi yao.

Hayo yamejiri leo Jumatatu bungeni jijini Dodoma wakati Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Dunstan Kitandula wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu CCM, Neema Mgaya aliyehoji  ni lini serikali itaondoa popo waliopo maeneo ya Upanga ili kulinda afya za wakazi wa maeneo hayo.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo, amesema Wizara imeendelea kuthibiti popo katika jiji la Dar-es-salaam kwa kuchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya ufuatiliaji kuangalia ukubwa wa tatizo.

Amesema kuna aina mbili ya popo wanaosumbua ikiwamo popo wanaotumia mapango au magofu ya nyumba kama makazi yao.

Amesema katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo, majaribio ya dawa tano za kunyunyizia ili kufukuza popo katika makazi yao zilitumika kati ya dawa hizo, dawa mbili(Napthalene na Bat CRP) zimeonekana kuwa na uwezo wa kuwafukuza popo hao na juhudi zaidi zinaendelea kwa kushirikiana na wadau kwenye maeneo husika.

“Utafiti huu umekamilika sasa jukumu lililopo mbele yetu ni wakuhakikisha kwamba wadau wote husika na kukubaliana na jambo hili, lipo kwenye halmashauri zetu zinachukua hatua za kuhakikisha kwamba tunasambaza dawa hizi kwa wananchi ili tuweze kukabiliana na tatizo hili. Niombe wadau wote husika tushirikiane ili tuweze kuondokana na tatizo hili,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!