Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mrithi wa Ali Bongo aapishwa, aahidi kurejesha madaraka kwa raia
Kimataifa

Mrithi wa Ali Bongo aapishwa, aahidi kurejesha madaraka kwa raia

Spread the love

JENERALI Brice Nguema, aliyemng’oa madarakani Rais wa Gabon, Ali Bongo katika mapinduzi ya kijeshi  yaliyofanyika wiki iliyopita, ameapishwa kuwa Rais wa mpito wa nchi hiyo kwa kipindi kisichojulikana. Anaripoti Isaya Temu, TUDARCo…(endelea).

Jenerali Nguema, amekula kiapo katika ikulu ya Rais leo tarehe 4 Septemba 2023, mbele ya chumba cha maafisa wa serikali, jeshi na viongozi wa eneo hilo katika mji mkuu wa Gabon, Libreville.

Hayo yamejiri ikiwa ni wiki moja  imepita baada ya Mapinduzi yaliyomngoa madarakani Rais Ali Bongo Odimba akiwa ni mmoja wa wanafamilia waliodumu madarakani kwa miaka 55.


“Naapa mbele za Mungu na watu wa Gabon kuulinda utawala wa Jamhuri kwa uaminifu,” ameapa Nguema.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya uapisho, Oligui amesema jeshi limechukua madaraka bila umwagaji damu na kuahidi kurejesha madaraka kwa wananchi kwa kuandaa uchaguzi huru, wa uwazi na wa kuaminika.

“Kwa serikali mpya, iliyoundwa na watu wenye uzoefu, tutampa kila mtu nafasi ya matumaini,” amesema.

Televisheni ya taifa ilionyesha picha za umati wa watu waliokuwa wakishangilia na vifaru vya Majeshi wakifyatua risasi baharini kuashiria furaha ya tukio hilo.

Hata hivyo pamoja na kutwaliwa kwa madaraka na Jeshi nchini Gabon bado kutasababisha kuendelea kwa utawala wa ukoo wa Bongo ambao umekuwa madarakani kwa miaka 55, chanzo kilicho karibu na Rais aliyeondolewa madarakani kimesema.

 

“Jenerali Brice Oligui Nguema ni zao la moja kwa moja la ukoo wa Bongo,” kilisema chanzo hicho, ambacho kilitaka kubaki bila kujulikana kwa sababu za kiusalama.

Jeshi nchini Gabon lilitangaza kuchukua madaraka hayo ya Urais muda mfupi baada ya Rais Ali Bongo kutangazwa mshindi wa uchaguzi uliokumbwa na utata.

Rais aliyepinduliwa bado yuko nyumbani kwake baada ya kuwekwa kizuizini na Jeshi wakati walipotwaa madaraka yake huku baadhi ya ndugu zake walikamatwa na uchunguzi unaendelea nchini Gabon pamoja na Ufaransa walipokimbilia baada ya mapinduzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!