MAOFISA wandamizi katika jeshi la polisi na taasisi nyingine za umma nchini Tanzania, wanatuhumiwa kusaidia mtandao wa wafanyabiashara wa dawa za kulevya nchini humo, kusafirisha, kuuza na kusambaza biashara hiyo haramu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa kutoka ndani ya serikali, jeshi la poli na mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, zimeeleza tayari vigogo kadhaa wanaotuhumiwa kwenye sakata hilo, wameanza kuhojiwa.
Miongoni mwa wanaotajwa, ni pamoja na viongozi wandamizi wa polisi, katika mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Kanda Maalum ya Dar es Salaam.
Mtoa taarifa wa Gazeti la Raia Mwema anasema, maofisa hao wanahojiwa kufuatia kuibuka kwa madai kumsaidia mmoja wa wafanyabiashara hao, anayejulikana kwa jina la Chrispin Pina, kuweza kuficha shehena kubwa ya madawa hayo.
Kwa habari zaidi, soma gazeti la Raia Mwema, toleo la leo Jumatano, tarehe 23 Juni 2021, kujua nini kilichotokea, bosi wa mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya alichokisema na kauli za Jeshi la Polisi – Mhariri.
Leave a comment