UMOJA wa Usafirishaji Abiria Mkoa wa Dar es Salaam, umependekeza bei ya nauli ipande kwa Sh. 400, ili kukabiliana na ongezeko la gharama za usafirishaji zilizochangiwa na kupanda kwa bei ya mafuta na kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania dhidi ya Dola ya Marekani. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Mapendekezo hayo yametolewa Katibu wa Umoja wa Usafirishaji Abiria Mkoa wa Dar es Dalaam (UWADAR), Selemani Kimomwe, katika kikao cha Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) cha kupokea maoni ya wadau juu ya bei za nauli.
“Kwa maoni yetu UWADAR tunaomba ongezeko la Sh. 400 la nauli kutoka kila nauli, mfano nauli ya Sh. 500 iongezeke kutoka Sh. 500 kuja Sh. 900, kwa ruti tu. Tunaamini maombi yetu yatafanyiwa kazi,” amesema Kimomwe.
Kimomwe amesema gharama za usafirishaji zimeongezeka hali iliyopelekea baadhi ya wamiliki kuondoa magari yao barabarani.
Ametaja baadhi ya gharama hizo ikiwemo ya faini zinazotozwa na mamlaka mbalimbali ikiwemo Jeshi la Polisi, pindi magari yao yanapokuwa chakavu kwa kushindwa kuyatengeneza.
“TANROADS tunalipa faini nyingi sana ambazo hazina msingi ukiangakia Jeshi la Polisi linapambana na sisi. Ukiangalia gharama inafikia kipindi inamuelemea mmilimi na kufanya asiweze kukiendesha,” amesema Kimomwe.
Kupanda kwa thamani ya dola inahusu nini dala dala? Kwani wao wanalipa mishahara kwa dola? Acheni uzandiki
Kama nauli ikipanda mara dufu je na mishahara ya watumiaji wa daladala itapanda?