KAMPUNI ya Gazprom, ambayo ni msambazaji mkuu wa gesi asilia nchini Urusi imesitisha usambazaji wa gesi kwa nchi za Bulgaria na Poland, baada ya nchi hizo kukataa kulipia nishati kwa ruble. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa Mashirika ya Kimataifa … (endelea).
Taarifa iliyotolewa leo jumatano tarehe 27 Aprili 2022 na kampuni hiyo, imesema kuwa Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema nchi ambazo, zinazoonekana sio rafiki kwa Urusi lazima zianze kulipia usambazaji wa gesi kutoka nchini humo kwa rubles.
Hata hivyo nchi zingine za Ulaya zimekataa kulipia kwa rubles, lakini hivi sasa ni nchi mbili ambazo Urusi imetangaza inasitisha Poland na Bulgaria.
Gazprom imewaonya Poland na Bulgaria,ikiwa wataamua kutumia gesi inayosafirishwa kwenda nchi zingine basi italazimika kupunguza kiwango hicho ambacho wataamua kuzuia kinyume cha sheria.
Leave a comment