Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi yaingilia kati mgogoro wa Hamas, Israel yataka ikae pembeni
Kimataifa

Urusi yaingilia kati mgogoro wa Hamas, Israel yataka ikae pembeni

Spread the love

 

NCHI ya Urusi, imeingilia kati mgogoro unaoendelea Palestina kwa kufanya mazungumzo na ujumbe wa kundi la wanamgambo wa kiislamu, Hamas, ili kutafuta namna ya kumaliza vita na Israel kwa njia ya amani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Tayari ujumbe wa Hamas, umeshawasili nchini Urusi kwa ajili ya kuzungumza na Serikali ya taifa hilo, ambalo halikitambua kikundi hicho kama cha kigaidi, tofauti na ilivyo kwa mataifa mengine.

Ujumbe huo ulioongozwa na Kiongozi Mkuu wa Hamas, Moussa Abu Marzouk, ulikutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Mikhail Bogdanov, kwa ajili ya mazungumzo.

Hata hivyo, Israel imeitaka Urusi kusitisha mazungumzo na Hamas, kwa madai kuwa imefanya mauaji ya maelfu ya waisrael wasiokuwa na hatia.

Tayari Shadi Barud, Naibu Mkuu wa kitengo cha kijasusi cha Hamas, aliyedaiwa kuhusika katika mipango ya tukio la uvamizi nchini Israel, lililosababisha mauaji ya amelfu ya watu, ameuawa.

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, taarifa hizo zimetolewa na Jeshi la Ulinzi la Israel, lililodai kuwa, Barud aliuliwa katika shambulio la anga lililofanywa na ndege za kivita.

Wakati mauaji ya kiongozi huyo wa Hamas aliyesuka uvamizi uliofanyika tarehe 7 Oktoba 2023 na kuzua mapigano yanayoendelea hadi sasa, mazungumzo ya kushawishi kundi hilo liwaache huru mateka wa Israel zaidi ya 220 yanaendelea.

Mtandao wa BBC Swahili umeripoti kuwa, wapatanishi kati ya Hamas na Israel wanaendelea na mzungumzo ya kusitiha mapigano kwa muda ili kuruhusu mateka hao waachwe huru hususan wanawake, watoto na wazee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Sakata la uhamiaji Rwanda lamng’oa waziri Uingereza

Spread the loveWaziri wa Uhamiaji wa Uingereza, Robert Jenrick amejiuzulu baada ya...

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

error: Content is protected !!