Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi yaingilia kati mgogoro wa Hamas, Israel yataka ikae pembeni
Kimataifa

Urusi yaingilia kati mgogoro wa Hamas, Israel yataka ikae pembeni

Spread the love

 

NCHI ya Urusi, imeingilia kati mgogoro unaoendelea Palestina kwa kufanya mazungumzo na ujumbe wa kundi la wanamgambo wa kiislamu, Hamas, ili kutafuta namna ya kumaliza vita na Israel kwa njia ya amani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Tayari ujumbe wa Hamas, umeshawasili nchini Urusi kwa ajili ya kuzungumza na Serikali ya taifa hilo, ambalo halikitambua kikundi hicho kama cha kigaidi, tofauti na ilivyo kwa mataifa mengine.

Ujumbe huo ulioongozwa na Kiongozi Mkuu wa Hamas, Moussa Abu Marzouk, ulikutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Mikhail Bogdanov, kwa ajili ya mazungumzo.

Hata hivyo, Israel imeitaka Urusi kusitisha mazungumzo na Hamas, kwa madai kuwa imefanya mauaji ya maelfu ya waisrael wasiokuwa na hatia.

Tayari Shadi Barud, Naibu Mkuu wa kitengo cha kijasusi cha Hamas, aliyedaiwa kuhusika katika mipango ya tukio la uvamizi nchini Israel, lililosababisha mauaji ya amelfu ya watu, ameuawa.

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, taarifa hizo zimetolewa na Jeshi la Ulinzi la Israel, lililodai kuwa, Barud aliuliwa katika shambulio la anga lililofanywa na ndege za kivita.

Wakati mauaji ya kiongozi huyo wa Hamas aliyesuka uvamizi uliofanyika tarehe 7 Oktoba 2023 na kuzua mapigano yanayoendelea hadi sasa, mazungumzo ya kushawishi kundi hilo liwaache huru mateka wa Israel zaidi ya 220 yanaendelea.

Mtandao wa BBC Swahili umeripoti kuwa, wapatanishi kati ya Hamas na Israel wanaendelea na mzungumzo ya kusitiha mapigano kwa muda ili kuruhusu mateka hao waachwe huru hususan wanawake, watoto na wazee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!