Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Ujenzi vyuo vya VETA washika kasi
Elimu

Ujenzi vyuo vya VETA washika kasi

Spread the love

KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Anthony Kasore, amesema Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa vyuo vya ufundi katika wilaya 25 na vya mikoa vinne, ili kukabiliana na changamoto ya wananchi kushindwa kushiriki kwenye shughuli za uchumi kutokana na kukosa ujuzi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).

Kasore amesema hayo eo tarehge 17 Oktoba 2023, akizungumzia maendeleo ya ujenzi wa chuo cha VETA Wilaya ya Igunga, mkoani Tabora, unaogharimu kiasi cha Sh. 2.6 bilioni, ambapo kikimalika kitahudumia wanafunzi 900 wa kozi za muda mfupi.

Kasore amesema mradi huo unaoendelea kutekelezwa nchi nzima na kugharimu Sh. 70.9 bilioni, umefikia asilimia 98, huku baadhi ya vyuo vikianza kutoa huduma.

“Mradi huu ulikuwa mahususi kutatua changamoto za shughuli za kiuchumi zinazotokea kwenye wilaya mbalimbali na kuhitaji wananchi kushiriki , lakini wameonekana wanakwama kwa kukosa ujuzi wa kushiriki. Serikali iliona vyema kujenga vyuo hivi na Serikali ilihakikisha vinamalizika na kutoa mafunzo,” amesema Kasore.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuTangulizi

Mwalimu Maganga Japhet asimamishwa kazi kwa utoro

Spread the loveMwalimu Maganga Japhet amesimamishwa kazi na Tume ya Utumishi wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Elimu

150 wahitimu Shahada ya Udaktari HKMU

Spread the loveCHUO Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU), kimeiomba serikali...

Elimu

Aliyehitimu udaktari HKMU na miaka 21 atoa siri

Spread the love MHITIMU wa fani ya udaktari ambaye ni mdogo kuwahi...

error: Content is protected !!