Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Ujenzi vyuo vya VETA washika kasi
Elimu

Ujenzi vyuo vya VETA washika kasi

Spread the love

KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Anthony Kasore, amesema Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa vyuo vya ufundi katika wilaya 25 na vya mikoa vinne, ili kukabiliana na changamoto ya wananchi kushindwa kushiriki kwenye shughuli za uchumi kutokana na kukosa ujuzi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).

Kasore amesema hayo eo tarehge 17 Oktoba 2023, akizungumzia maendeleo ya ujenzi wa chuo cha VETA Wilaya ya Igunga, mkoani Tabora, unaogharimu kiasi cha Sh. 2.6 bilioni, ambapo kikimalika kitahudumia wanafunzi 900 wa kozi za muda mfupi.

Kasore amesema mradi huo unaoendelea kutekelezwa nchi nzima na kugharimu Sh. 70.9 bilioni, umefikia asilimia 98, huku baadhi ya vyuo vikianza kutoa huduma.

“Mradi huu ulikuwa mahususi kutatua changamoto za shughuli za kiuchumi zinazotokea kwenye wilaya mbalimbali na kuhitaji wananchi kushiriki , lakini wameonekana wanakwama kwa kukosa ujuzi wa kushiriki. Serikali iliona vyema kujenga vyuo hivi na Serikali ilihakikisha vinamalizika na kutoa mafunzo,” amesema Kasore.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!