Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tume kudhibiti vigogo kuchafuliwa mitandaoni yazinduliwa
Habari za Siasa

Tume kudhibiti vigogo kuchafuliwa mitandaoni yazinduliwa

Spread the love

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amezindua Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, yenye jukumu la kudhibiti uvujaji wa taarifa za faragha za watu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Uzinduzi wa tume hiyo pamoja na mifumo ya usajili wa malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya ulinzi wa taarifa binafsi, umefanywa na Rais Samia leo tarehe 3 Aprili 2024, jijini Dar es Salaam.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akigusa screen ya iPad kuashiria uzinduzi wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi pamoja na mifumo ya usajili na malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya ulinzi wa taarifa binafsi katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 3 Aprili 2024.

Mkuu huyo wa nchi amesema tume hiyo itasaidia kulinda taarifa za watanzania katika sekta ya kiuchumi, kijamii na kisiasa huku akidai itasaidia kuwadhibiti wanasiana wanaozitumia taarifa za watu vibaya mitandaoni kwa lengo la kujipatia mamlaka.

“Sheria ya ulinzi binafsi na tume ya kulinda taarifa binafsi ni nyenzo muhimu katika kujenga uchumi na mifumo ya kidigitali. Niseme tunapoizindua tume hii itambue kwamba ina kazi nzito sana na ni muhimu kwa maisha yetu ya kijamii, kisiasa na kiuchumi,”

“Mifumo yake mnayokwenda kusimamia inaweza kutumika kukuza uchumi wa kidigitali na kisiasa kwa wanaotaka mamlaka wakaitumia hiyo mifumo ya kisiasa wakawasema wengine wakapenya,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema tume hiyo itasaidia kudhibiti watu au vikundi vinavyodukua taarifa za watu binafsi, kwa kuwa itakuwa na jukumu la kukusanya na kutunza taarifa hizo.

“Kila mwanadamu ana utashi na anastahili staha, hivyo zipo baadhi ya taarifa asingependa kujulikana kwa kila mtu, kwa kweli ingekuwa taarifa zetu zote ziko wazi na watu wanazijua tusingetazamana usoni au hii dunia ingekuwa ya aina nyingine. Hakuna faragha hakuna staha lakini kwa sababu mwanadamu anahitaji staha ndio maana tumekuja na tume hii,” amesema Rais Samia.

Rais Samia ameagiza taasisi za umma na vinafsi zinasajiliwa katika mfumo wa tume hiyo kabla ya Disemba 2024.

Miongoni mwa majukumu ya tume hiyo, ni kufanyia kazi malalamiko ya haki ya faragha kisha kuwachukulia hatua wahusika watakaobainika kutenda kosa hilo.

Lengo lingine ni kudhibiti taasisi zinazohusika na utunzaji wa taarifa binafsi, kutotoa siri za wateja wao hadharani kinyume cha sheria, kwa ajili ya maslahi yao binafsi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!