Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Michezo TFF yaridhia ombi la Yanga, Ninja kuivaa Simba
Michezo

TFF yaridhia ombi la Yanga, Ninja kuivaa Simba

Spread the love

KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) chini ya Mwenyekiti wake Wakili, Kiomoni Kibamba imeridhia ombi la Yanga kuahirisha kusikiliza shauri dhidi ya mlinzi wa kati wa timu hiyo Abdallah Shaibu ‘Ninja’ katika kikao kilichofanyika Februari 9, 2019. Anaripoti Kelvin Mwaipungu …  (endelea)

Yanga waliomba kamati hiyo ya nidhamu kusogeza mbele shauri la mchezaji wao kutokana kuwa na timu katika mechi za mikoani ya Ligi Kuu hivyo na kuombwa lisikilizwe katika kikao kijacho.

Mchezaji huyo aliitwa mbele ya kamati hiyo wiki moja iliyopita mara baada ya bodi ya ligi kupeleka malalamiko ndani ya TFF kuhusu Ninja kuonesha vitendo visivyo vya uungwana kwenye mchezo dhidi ya Coastal Union kutoka Tanga.

Ninja alionekana kumpiga kiwiko mchezaji Andrew Simchimba kwenye mchezo uliofanyika tarehe 3, Februari, 2019 kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga na mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Kwa maana hiyo mchezaji huyo anatakiwa kwenda kujitetea au kutuma mwakilishi kwenye kikao kijacho na baadaye kamati hiyo kutoa maamuzi juu ya shauri hilo.

 

 

 

 

 

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

error: Content is protected !!