Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu TCU wapiga ‘stop’ udahili vyuo vikuu
Elimu

TCU wapiga ‘stop’ udahili vyuo vikuu

Katibu Mtendaji TCU, Charles Kihampa
Spread the love

TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imezuia udahili wa wananfunzi wapya katika vyuo vikuu vinne  pamoja na kuamuru wanafunzi wake wa shahada ya kwanza kwa mwaka wa masomo wa 2018/19 kwenye programu tisa kuhamishiwa katika vyuo vingine. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Katika hatua nyingine, TCU imefuta usajili wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Kumbukumbu ya Stefano Moshi (SMMUCo) na kuamuru wanafunzi wa chuo hicho wanaoendelea na masomo wahamishiwe kwenye kampasi kuu ya SMMUCo iliyopo Masoka wilayani Moshi mkoa wa Kilimanjaro.

Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa akizungumza na wanahabari leo tarehe 9 Novemba 2018, amevitaja vyuo vinne vilivyozuiliwa udahili ikiwemo Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU), Chuo Kikuu Kishiriki cha Askofu Mkuu James (Ajuso), na Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastiano Kolowa (SEKOMU).

Prof. Kihampa amesema, chuo cha IMTU kilichopo jijini Dar es Salaam, kimezuiliwa kudahili wanafunzi wa program ya shada ya tiba na upasuaji, shahada ya uuguzi na sayansi, wakati Ajuco cha Songea mkoani Ruvuma kikizuiwa kudahili wanafunzi wa udaktari wa binadamu.

Huku SEKOMU kilichopo wilayani Lushoto mkoa wa Tanga, kikizuiliwa kudahili wanafunzi wa program za shada ya sayansi na elimu, shahada ya sheria na shahada ya elimu na mahitaji maalumu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!