Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Simba kuivaa Mbabane Swallows Klabu Bingwa Afrika
Michezo

Simba kuivaa Mbabane Swallows Klabu Bingwa Afrika

Patrick Aussems, Kocha Mkuu wa Simba
Spread the love

MABINGWA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba watamenyana dhidi ya Mbabane Swallows katika hatua ya awali ya michuano ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika, inayotarajiwa kuanza mwisho wa mwezi Novemba. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Mchezo huo unaotarajiwa kuchezwa kati ya tarehe 27-28 mwezi huu katika mzunguko wa kwanza ambao Simba wataanzia nyumbani, huku mchezo wa marudiano ukitarajia kupigwa kati ya tarehe 4-5.

Ikumbukwe Mbabane Swallows ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Swaziland walifanikiwa kuiondosha Azam FC katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika 2017, licha ya sasa kushika nafasi ya nne kwenye msimamo la ligi kuu nchini humo wakiwa na alama 16, baada ya kucheza michezo 8.

Simba watawavaa mabingwa hao baada ya kutoshiriki michuano ya klabu bingwa barani Afrika kwa misimu mitano, toka walivyofanya hivyo mwaka 2012 baada ya kuibuka mabingwa katika msimu wa 2011/12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!