Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaridhia kufanya Uchaguzi
Michezo

Yanga yaridhia kufanya Uchaguzi

Jengo la Yanga
Spread the love

KLABU ya Yanga kupitia kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wameanza zoezi la uchukuaji fomu kwa ajili ya kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi zilizo achwa wazi za viongozi wa wawili na wajumbe wanne wa kamati ya utendaji kufuatia kujiuzuru kwao. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Uchaguzi huo unatarajia kufanyika 11 Januari, 2019 utakuwa katika nafasi ya Mwenyekiti, Kaimu Mwenyekiti na wajumbe wanne wa kamati ya utendaji ambapo zoezi la uchukuaji fomu limeanza leo katika ofisi za TFF pamoja na klabu ya Yanga huku mwisho wake ukiwa tarehe 13 Novemba, 2018.

Yanga wameamua kuingia katika mchakato huu baada ya kikao kilichofanyika kati yao na uongozi wa shirikisho baada ya kutokea kwa mvutano kufuatia baraza la Michezo Tanzani (BMT) kuwataka klabu hiyo kufanya uchaguzi wa kuziba nafasi hizo huku wakisimamiwa na kamati ya uchaguzi wa TFF.

Akizungumzia mchakato huo Kaimu Mwenyekiti wa Yanga ambaye ameteuliwa na Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, Thobias Lingalangala hadi hapo uchaguzi wa kujaza nafasi utakapofanyika Januari 13 amesema kuwa uchaguzi utafanyika kama ulivyotangazwa na kamati ya uchaguzi ya TFF.

“Baada ya kikao cha jana kati yetu na TFF ambao ni wasimamizi wetu hakuna tena kikao kingine kilichopangwa kwa sababu tupo kwa ajili ya kutekeleza katiba ya Yanga, taratibu za TFF na FIFA lakini chini ya Serikali yetu hivyo baada ya kikao hicho kinacho fuata ni uchaguzi,” alisema Thobiasi Lingalangala.

Aidha Lingalangala aliongezea kuwa kumekuwa na mambo mengi ya kutaka kuchelewesha uchaguzi kwa baadhi ya wanachama na hivyo kama mtu ana mapenzi na kiongozi yoyote ndani ya Yanga basi amshawishi au amchukulie fomu agombe.

“Kama kuna mtu ana mapenzi na Mwenyekiti Loid Nchunga basi amchukulie fomu agombee, kama kuna mtu ana mapenzi na Francis Kifukwe basi amshawishi amchukulie fomu agombee, kama kuna mtu ana mapenzi na Mwenyekiti Imani Madega basi amshawishi agombee na kama kuna mtu ana mapenzi na Yusuph Manji basi amshawishi na amchukulie fomu agombee”

Gharama za fomu hizo katika nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti itakuwa shilingi 200,000 na wajumbe kamati ya utendaji itakuwa shilingi 100,000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!