Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tanzania yashtakiwa kesi 13, yadaiwa dola 185 milioni
Habari za Siasa

Tanzania yashtakiwa kesi 13, yadaiwa dola 185 milioni

Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi
Spread the love

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amebainisha kuwa, mashauri 13 yenye jumla ya madai kiasi cha dola za Marekani 185.5 Milioni, yamefunguliwa dhidi ya serikali katika mahakama za kimataifa za usuluhishi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni jijini Dodoma leo tarehe 9 Novemba 2018, Prof. Kabudi amesema kesi hizo zimefunguliwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi ya London (LCIA), Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) na Mahakama ya Kudumu ya Usuluhishi (PCA) kuanzia mwezi Novemba 2015 hadi mwaka huu.

“Mashauri yaliyofunguliwa nje ya nchi dhidi ya serikali kuanzia Novemba 2015 ni 13, aidha mashauri hayo yapo katika mahakama mbalimbali za usuluhishi ikiwemo (PCA), (LCIA) NA (ICSID) na huko Johannesburg Afrika Kusini. Jumla ya madai ya kesi hizo ni dola za kimarekani 185,580,009.76,” amesema Prof. Kabudi.

Aidha, amesema mashauri yote yaliyopo kwenye mahakama za kimataifa bado hayajatolewa uamuzi, hivyo takwimu halisi za madai na gharama ambazo serikali inaweza kuwajibika kulipa itapatikana baada ya mashauri husika kukamilika na uamuzi kutolewa.

Prof. Kabudi ametoa takwimu hizo akijibu swali la Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe aliyetaka kujua tangu mwaka 2015 hadi sasa Tanzania imefunguliwa mashauri mangapi katika mahakama za kimataifa kuhusiana na masuala ya uwekezaji na mikataba ya kibiashara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!