Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Michezo Taswa wampongeza Mobhare Matinyi
Michezo

Taswa wampongeza Mobhare Matinyi

Mobhare Matinyi
Spread the love

 

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kinampongeza Mobhare Matinyi kwa kuaminiwa na kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Uteuzi wa Matinyi aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa TASWA, umefanywa jana Oktoba mosi, 2023 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Kabla ya uteuzi huo ulioanza mara moja, Matinyi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam.

Matinyi ambaye kitaaluma ni Mwandishi wa Habari na Mwanadiplomasia mbobevu aliyewahi kufundisha Chuo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dk. Salim Ahmed Salim, Kurasini jijini Dar es Salaam aliwahi kuwa Mwenyekiti wa TASWA kwa mafanikio makubwa.

TASWA tunamtakia kila la kheri katika nafasi hiyo aliyoaminiwa na Mheswhimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye pia anastahili pongezi kwa uteuzi huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Pesa ipo huku Meridianbet, beti sasa

Spread the love  WIKIENDI inaishia leo hii jaman kama bado hujasuka mkeka...

Michezo

Wenzako wameshakuwa mamilionea hapa wewe unasubiri nini?

Spread the love  WIKIENDI imefika na ukiachana na mvua za Dar es...

Michezo

Manchester City vichwa chini Ligi Kuu England

Spread the love MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Uingereza klabu yaManchester City...

Michezo

Piga mkwanja wa kutosha katika usiku wa kibabe kati ya Man United vs Chelsea

Spread the love USIKU wa leo katika dimba la Old Trafford utapigwa mchezowa...

error: Content is protected !!