Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Taswa wampongeza Mobhare Matinyi
Michezo

Taswa wampongeza Mobhare Matinyi

Mobhare Matinyi
Spread the love

 

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kinampongeza Mobhare Matinyi kwa kuaminiwa na kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Uteuzi wa Matinyi aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa TASWA, umefanywa jana Oktoba mosi, 2023 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Kabla ya uteuzi huo ulioanza mara moja, Matinyi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam.

Matinyi ambaye kitaaluma ni Mwandishi wa Habari na Mwanadiplomasia mbobevu aliyewahi kufundisha Chuo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dk. Salim Ahmed Salim, Kurasini jijini Dar es Salaam aliwahi kuwa Mwenyekiti wa TASWA kwa mafanikio makubwa.

TASWA tunamtakia kila la kheri katika nafasi hiyo aliyoaminiwa na Mheswhimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye pia anastahili pongezi kwa uteuzi huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!