Wednesday , 6 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka
Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia kupokea ndege mpya ya masafa ya kati aina ya Boeng 737-9, ya Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL), pamoja na ndege mbili ndogo za mafunzo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 2 Oktoba 2023, jijini Dar es Salaam na Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa ambapo hafla ya mapokezi hayo itafanyika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini humo.

Prof. Mbarawa amesema ndege hizo ni miongoni mwa ndege nne mpya ambazo Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, iliingia mkataba na Kampuni ya Boeng ya Marekani, kwa ajili ya utengenezaji Julai 2021.

Ndege hizo ni mbili za abiria za masafa ya kati aina ya Boeng 737-9 yenye uwezo wa kubeba abiria 181 kila moja, ndege moja ya abiria ya masafa marefu ya Boeng 787-8 Dreamliner (abiria 262) na ndegemoja kubwa ya mizigo ya Boeng 767-300 yenye uwezo wa kubeba tani 54.

Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa

“Serikali yetu chini ya uongozi mahiri wa Rais Samia, imeendelea kuhakikisha kuwa ATCL inatoa huduma zenye kuhimili ushindani kwa kuanzisha safari za moja kwa moja kwenda kwenye masoko ya kikanda na kimataifa,” amesema Prof. Mbarawa.

Waziri huyo wa uchukuzi amesema kuwasili kwa ndege hiyo ya abiria kutafanya idadi ya ndege za ATCL kuongezeka kutoka 13 hadi 14. Amesema ndege nyingine mbili zilizosalia zinaendelea kutengenezwa nchini Marekani, zinatarajiwa kuwasili nchini Desemba 2023 na Machi 2024.

Amesema ujio wa ndege hiyo, kutaifanya ATCL kuhudumia vituo vya ndani 14, vituo vya kikanda na kimataifa vikiwemo vya Nairobi (Kenya), Bunjumbura (Burundi), Ndola na Lusaka (Zambia), Lubumbashi (DRC).

“Utasaidia kuongeza miruko ya safari za usiku kwa viwanja vya ndege vyenye taa, kuanzisha safari za usiku katika viwanja vya ndege vya Dodoma na Songea, ambapo miradi ya ufungaji taa inakamilika. Aidha, ATCL itaendelea na miruko yake ya kimataifa na itaanzisha safari mpya za Goma, Lagos Nigeria,” amesema Prof. Mbarawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bashungwa: Katesh kutafanyiwa usafi wa hali ya juu

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema kazi ya kuondoa tope...

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

BiasharaTangulizi

Bei ya Dizeli, Petroli yashuka

Spread the loveBEI ya mafuta kwa mwezi Disemba, imeshuka kutokana na kupungua...

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!