Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tanzania, Indonesia zasaini mikataba minne ya ushirikiano
Habari za Siasa

Tanzania, Indonesia zasaini mikataba minne ya ushirikiano

Spread the love

JAMHURI ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Indonesia zimesaini mikataba minne ya ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Mikataba hiyo imesainiwa leo tarehe 25 Januari 2024, jijini Jakarta nchini Indonesia mbele ya Rais wa taifa hilo, Joko Widodo na Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ambaye yuko katika ziara ya kikazi kuanzia jana hadi tarehe 26 Januari mwaka huu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Joko Widodo katika Ofisi za Rais huyo Bogor Presidential Palace tarehe 25 Januari 2024.

Mikataba iliyosainiwa ni ya ushirikiano katika ukuzaji ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Indonesia, sekta ya kilimo, madini, uchumi wa buluu hususan kwenye uvuvi na usafiri wa majini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Samia alisema mikataba hayo ni matokeo ya pande zote mbili kuridhishwa na makubaliano yaliyowekwa Agosti 2023 Rais Widodo alipowasili Tanzania kwa ziara ya kikazi.

“Tulijadili ujio wa Rais Widodo Agosti 2023 na kuridhishwa na utekelezaji wa maazimio tuliyokubaliana pande zote mbili na kukubalia kuongeza zaidi utekelezaji. Tumesisitiza kuendelea kushirikiana kukuza ushirikiano katika uwekezaji baina ya nchi zetu mbili na baadae nitashiriki jukwa la biashara kati ya jumuita ya wafanyabiashara wa Indonesia na Tanzania,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!