Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Taifa Stars yatua salama, yapokelewa kwa shangwe na mashabiki
Michezo

Taifa Stars yatua salama, yapokelewa kwa shangwe na mashabiki

Spread the love

TIMU ya Taifa ya Mpira wa Miguu (Taifa Stars) imetua salama alfajiri ya leo tarehe 9 Septemba 2023 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ikitokea nchini Algeria kwenye mchezo wa kufuzu mashindano ya AFCON 2023 yatakayochezwa mapema mwakani 2024 nchini Ivory Coast. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Katika mchezo huo uliochezwa tarehe 7 Septemba 2023, Tanzania na Algeria zilitoka zilitoka sare ya bila kufungana (0-0), matokeo ambayo yanazifanya timu hizo kufuzu michuano hiyo, huku Tanzania ikifuzu kwa mara ya tatu katika historia ya mashindano hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutua jijini Dar es salaam, Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Saidi Yakubu ambaye aliongoza msafara wa timu hiyo kwa niaba ya Serikali, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa maono yake kwenye sekta ya michezo, hamasa pamoja na kuunga mkono timu hiyo.

Aidha, amewashukuru Watanzania wote kwa sala, dua na maombi yao na kuiunga mkono timu yao ya Taifa na kusisitiza kutakuwa na utaratibu mzuri kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) hatua itakayowezesha mashabiki waende kwa wingi nchini Ivory Coast mwakani 2024 kwenye michuano hiyo ili kuendelea kupeperusha vyema bendera ya taifa.

“Wizara yetu ambayo inaongozwa na Waziri Dk. Damas Ndumbaro itaendelea kuyaishi maono ya rais katika kuiendeleza wa timu ya Taifa na sasa ufadhili na uangalizi utaongezeka zaidi ili Ivory Coast tukafanye vizuri zaidi” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!