Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Silaa: Mkataba umetaja maeneo machache, tz nzima
Habari za Siasa

Silaa: Mkataba umetaja maeneo machache, tz nzima

Spread the love

MBUNGE wa Ukonga, Jerry Silaa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC), amesema mkataba wa uwekezaji katika bandari nchini baina ya Serikali ya Tanzania na Dubai umetaja maeneo machache mahususi ya ushirikiano na sio nchi nzima. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumza katika Kituo cha runinga cha Clouds leo Ijumaa amesema; “Tumesema IGA hii ni mkataba baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa niaba ya Tanzania na Falme ya Dubai na ibara ya 2 (1) inaeleza kuwa nia hasa ni kutengeneza msingi wa kisheria wa ushirikiano.

“Sasa huo ushirikiano unatajwa ibara ya 4 (1) kwa awamu ya kwanza na ya pili, na kinachotajwa ni ushirikiano sio miradi. Ukienda 5 (1) ndio inaeleza miradi itakayoanza ni ipi, ambayo ni Bandari ya Dar maeneo 7. Lakini mtu anakuja kukuambia yako maeneo 54, mpaka unapata tabu kwa sababu hayapo.

Aidha, amesema hakuna ibara inayoonesha kuwa bandari hiyo imeiuzwa.

“Wanaosema bandari inauzwa, waonyeshe watu mahali panaposema mauziano, kwa sababu hata ibara ya 12 (1) inaongelea mambo ya ulinzi katika mkataba huu wa uwekezaji wa bandari na wala sio kuuziana kama watu wanavyojaribu kusema” amesema na kuongeza kuwa;

“Watanzania wote wana haki ya kuzungumzia mkataba huu, lakini lazima tuuweke kisheria. Bahati mbaya katika wapotoshaji hawa wakati mwingine hawatumii hoja za msingi jambo linalopoteza maana ya majadiliano mitaani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!