Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shule zote Tanzania kufunguliwa Juni 29
Habari za SiasaTangulizi

Shule zote Tanzania kufunguliwa Juni 29

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli ameagiza shule zote nchini humo zifunguliwe tarehe 29 Juni 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea),

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo Jumanne tarehe 16 Juni 2020 wakati akihutubia Bunge jijini Dodoma.

Amesema, hali ya maambukizi ya ugonjwa wa vurusi vya corona (Covid-19) yamepungua.

Pia, Rais Magufuli ameagiza shunguli zingine nazo zirejee, “maisha ni lazima yarudi kama yalivyokuwa zamani.”

Shule hizo zilifungwa tangu tarehe 17 Machi 2020 ili kuepuka maambukizo ya corona.

Jana Jumatatu tarehe 15 Juni 2020, Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa alihitimisha mkutano wa 19 wa Bunge hilo la 11, alisema maambukizi hayo yamepunguza na wagonjwa waliopo ni 66 pekee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!