Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Uchaguzi utakuwa huru kwa vyama vyote lakini…
Habari za Siasa

Rais Magufuli: Uchaguzi utakuwa huru kwa vyama vyote lakini…

Sanduku la kura
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amesema, Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020 utafanyika kwa amani, huru na haki huku akionya yeyote atakayethubutu kuuvuruga atachukuliwa hatua kali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumanne tarehe 16 Juni 2020 wakati akilivunja Bunge la 11 la Tanzania.

Kuvunjwa kwa Bunge hilo alilolizindua tarehe 20 Novemba 2015, kunatoa fursa ya kuanza rasmi kwa mchakato wa uchaguzi mkuu.

Rais Magufuli amesema, “tumejipanga kuhakikisha uchaguzi huu, unakuwa huru na haki.”

“Tutasimamia uchaguzi huru na haki kwa vyama vyote na hii ndiyo demokrasia ya kweli. Vyama vya siasa na wanasiasa kujiandaa vizuri katika uchaguzi huu,” amesema huku akishangiliwa na wabunge.

Rais John Magufuli

Rais Magufuli ametumia fursa hiyo kuvisihi vyama vya siasa , “kutoa fursa kwa wanawake, vijana na wenye ulemavu.”

Kiongozi huyo mkuu amewasihi wananchi kuepuka pepo la, “matusi na kejeri, matusi na kejeri hayajengi. Sisi sote ni wamoja, tukabishane kwa hoja na kushindanisha ilani yetu.”

Akihitimisha eneo hilo la uchaguzi, Rais Magufuli amesema, “kwa yoyote atakayetaka kuleta vurugu katika uchaguzi huu, namtahadharisha kwamba Serikali iko macho.”

Rais Magufuli amelivunja Bunge hilo hadi pale litakapoitishwa tena kwa mujibu wa sheria.

1 Comment

  • Usije ukawa kama ule uchaguzi wa mitaa kwa sababu katika folu waliandika St badala ya Street

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!