RAIS John Magufuli amepiga ‘stop’ kufanyika Sherehe za Uhuru mwaka huu. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa amesema hayo leo Jumanne na kwamba, kila mkoa na wilaya watasherehekea kwa namna watavyopanga kwenye maeneo yao.
Waziri Majaliwa amesema kuwa, Rais Magufuli ameagiza pesa ambazo ni zaidi ya Sh. 900 milioni zingetumika kwenye sherehe hizo zitaelekezwa kwenye ujenzi wa hospitali.
Hospitali hiyo inatarajiwa kujengwa jijini Dodoma itakayoitwa Hospitali ya Uhuru.
Sherehe za Uhuru hufanyika tarehe 9 Desemba kila mwaka.
Leave a comment