SERIKALI imewapa unafuu wakaazi wa nyumba mpya za Magomeni Kota kwa kuwawezesha kununua nyumba hizo kwa mfumo wa mpangaji mnunuzi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Nafuu hiyo imetolewa na Rais Samia Suluhu leo Jumatano Tarehe 23 Machi 2022, wakati akizundua nyumba hizo na kukabidhi funguo kwa kaya 644.
Wakaazi hao kwa mujibu wa makubaliano wataishi katika nyumba hizo kwa miaka mitano bure ili kufidia gharama walizotumia kuishi nje ya makazi yao baada ya nyumba zao kubomolewa.
Hata hivyo, Rais Samia amewashauri wakaazi hao kuanza kulipa fedha hizo kidogo kidogo kuanzia sasa badala ya kusubiri miaka mitano ili kupunguza mzigo.
Mbali na nafuu hiyo ya ununuzi pia Serikali imewapa muda wa mapumziko ya kutochangia huduma kwa kipindi cha miezi mitatu.
Amewataka wakaazi hao kuzitunza nyumba hizo kwa kuzingatia usafi wa maeneo yanayowazunguka ili ziweze kudumu.
Leave a comment