RAIS Samia Suluhu Hassan amesema watu wanaofikiri kwamba miadi iliyoachwa na mtangulizi wake haitaendelezwa wana upeo mdogo wa kufikiri. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 23 Machi 2022, akizundua nyumba za Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.
Amesema waliokuwa wanasema hivyo hawakuwa hata na sababu na kubainisha kuwa hakuna sababu ya miradi kutoendelea kwasababu imeagizwa katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Serikali zote zinazoongoza Tanzania ni za Chama Cha Mapinduzi awamu moja ikiondoka awamu ya pili inashika Serikali… kwahiyo wanaposema kwamba miradi haitatekelezwa nadhani upeo wao wa kufikiri ni mdogo sana,” amesema na kuongeza;
“Hata miradi hii ilivyoanzishwa awamu ya tano mimi nilikuwa Makamu wa Rais kwahiyo ni sehemu ya miradi hiyo kuanza kwake na kutekelezwa kwake.
“Lakini kwa kunitazama sura na kusema asingeweza kuendeleza hii miradi haikuwa busara, lakini tuwaombee nasi tujiombee Mungu atupe nguvu na busara zaidi miradi hii iendelee kwa maendeleo ya nchi yetu.
Leave a comment