Tuesday , 30 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yapata hasara 113 milioni hospitali kuwapa misamaha wagonjwa wasiostahili
Habari Mchanganyiko

Serikali yapata hasara 113 milioni hospitali kuwapa misamaha wagonjwa wasiostahili

Hospitali ya Sekou Toure
Spread the love

SERIKALI imepata hasara ya kiasi cha Sh. 111.76 milioni, baada ya baadhi ya hospitali za rufaa za mikoa kutoa msamaha wa matibabu kwa watu wasiokuwa na sifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamebanishwa katika ripoti ya ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, kwa mwaka wa fedha wa 2022/23, iliyowasilishwa jana Jumatatu, bungeni jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa ukaguzi huo, imebanika hospitali tatu za rufaa zilitoa misamaha kwa wagonjwa wasiostahili, Mount Meru ilitoa msamaha wa Sh. 25.36 milioni, Sekou Toure (Sh. 7.29 milioni) na Songwe (Sh. 79.09 milioni).

“Ukaguzi ulibaini hospitali tatu za rufaa za mikoa hazikukusanya jumla ya Sh. milioni 111.76, baada ya kutoa misamaha ya gharama za matibabu kwa wagonjwa wasio na sifa ikijumuisha misahama ya matibabu ya wafungwa na watu wengine bila kuwepo kwa nyaraka za kuthibitisha vigezo vilivyotumika,” imesema ripoti hiyo na kuongeza:

“Badala yake, hospitali hizi zilipaswa kuwasilisha hati za madai ya gharama za matibabu ya wafungwa katika idara husika ya Magereza (Fungu 29). Upotevu huu wa mapato unasababishwa na kutofanyika kwa tathmini ya vigezo vya utoaji wa misamaha ya gharama za matibabu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari Mchanganyiko

Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba

Spread the love MKUU wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Kennan Kihongosi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

error: Content is protected !!