SERIKALI imesema imeondoa dawa 178 katika kitita cha Mfuko wa Taifa wa Bima (NHIF), ili kupisha dawa bora zaidi zinazoendana na wakati wa sasa kwa magonjwa yote yanayowakumba watanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Ufafanuzi huo umekuja siku chache baada ya kuibuka vute ni kuvute kuhusu matumizi ya kitita hicho kilichohuishwa tarehe 18 Disemba mwaka jana na kupingwa na baadhi ya wamiliki wa hospitali binafsi.
Akitoa ufafanuzi leo Jumamosi Mkurugenzi wa Huduma za Dawa na Mfamasia Mkuu wa Serikali Daudi Msasi amesema baadhi ya dawa hizo zimeondolewa katika muongozo huo wa matibabu ili kuepuka uandishi wa dawa zenye muunganiko yaani Fixed Dose Combonation kwa kuwa nyingi zinakuwa zimebeba majina ya kibiashara.
Amesisitiza kuwa mwongozo huo umezingatia upatikanaji wa dawa zote muhimu kwa magonjwa yote nchini na kwa ngazi zote kuanzia Zahanati hadi Hospitali ya Taifa.
Baadhi ya dawa zilizoondolewa ni zile zinazotibu magonjwa ya presha na sukari na wenye matatizo ya moyo.
Dawa za malaria kadhaa aina ya Artemether za vidonge, sindano na dripu pia zimeondolewa kwenye kitita hicho pamoja na dawa ya vidonge ya chloroquine inayotibu wenye selimundu.
Leave a comment