Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Maisha Afya Serikali kuwatibu wagonjwa damu nchini
Afya

Serikali kuwatibu wagonjwa damu nchini

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imesema inafanya mkakati wa kuhakikisha watanzania wote wanaougua magonjwa ya damu watibiwe ndani ya nchi kwa kujengea uwezo hospitali zote nchini. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Mganga Mkuu wa serikali Prof. Muhammad Bakari amesema magonjwa hayo ni kama SeliMundu, Upungufu wa damu na Kansa ya damu.

Amesema kuwa lengo la kufanyika kwa mafunzo hayo ni kuhakikisha kunakuwepo na uwezo wa kutibu wagonjwa ndani ya nchi unaimarika.

“Kinachofanyika hapa ni kitu muhimu sana kwetu, kwasababu wataalam wetu wanapata ujuzi mkubwa zaidi kwenye magonjwa ya damu na upatikanaji wa damu na ni heshika kwetu kama nchi kwasababu ni mara ya kwanza yanafanyika nchini kwetu,” amesema.

Aidha Makamu wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, Prof Andrea Pembe amesema kuwa kwa idadi ya watoa huduma ya afya Tanzania ni chache ukilinganisha na iddi ya Watanzania wote hivyo nguvu kubwa inahitajika kuongeza watoa huduma katika vituo vya afya.

Amesema kuwa Hospitali za Kanda na Rufaa zina upungufu wa madaktari bingwa na zinahitaji takriban zaidi ya 500 ambapo ni asilimi 79.

“Serikaali kwa ujumla imekuwa ikijitahidi kutoa ufadhiri kwa watu ili waende wakasome lakini kutokana na uwezo wa kusomesha kuwa mdogo hivyo inakuwa ngumu kufanya hivyo,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi GGML wajitokeza kuchunguzwa saratani

Spread the loveWAFANYAKAZI wa Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) leo...

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML yatoa msaada wa vifaa tiba kuboresha afya Geita

Spread the loveKATIKA jitihada za kuendelea kuboresha sekta ya afya mkoani Geita,...

Afya

Hospitali Kanda Mtwara yaokoa mamilioni, yajipanga kuhudumia nchi jirani

Spread the love  MAMILIONI ya fedha yaliyopaswa kutumika katika kusafirisha wagonjwa kutoka...

AfyaHabari Mchanganyiko

Magonjwa yasiyoambukiza tishio, vyombo vya habari vyatakiwa kuelimisha umma

Spread the loveVYOMBO vya habari vimetakiwa kuongeza jitihada katika elimu ya kujikinga...

error: Content is protected !!