Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Saprong, Kisinda waanza kwa furaha Yanga
Michezo

Saprong, Kisinda waanza kwa furaha Yanga

Spread the love

BAADA ya kupachika mabao mawili kwenye mchezo wa jana Jumapili tarehe 30 Agosti 2020 dhidi ya Aigle Noir ya Burundi kwenye kilele cha ‘Wiki ya Mwananchi’ mshambuliaji Michael Sarpong na winga Tuisila Kisinda wa Yanga, wameanza vizuri kwenye mchezo wao wa kwanza toka walipojiunga na timu hiyo kwenye dirisha kubwa la usajili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)

Mchezo huo ambao ulikuwa wa kirafiki na kama sehemu ya tamasha hilo, viwango vya nyota hao wawili vilionekana kuwavutia mashabiki wengi wa klabu hiyo ambao walionekana kutegemea makubwa kutoka kwao katika kurudisha heshima yao ya ubingwa kwa msimu huu ambao wameukosa kwa  miaka mitatu mfululizo.

Bao la kwanza la Yanga katika mchezo huo, lilifungwa na Tuisila Kisinda dakika ya 38 na baadae katika kipindi cha pili, Michael Sarpong alipachika bao la pili 51 kwa kichwa baada ya kupokea pasi kutoka kwa Ditram Nchimbi.

Katika mchezo huo, Kisinda alionekana kuvutia mashabiki wengi wa Yanga kutokana na kasi yake uwanjani na uwezo mkubwa wa kufunga pale anapopata nafasi.

Kwa upande wa Sarpong alionekana kuwa msumbufu kwa walinzi wa timu pinzani kutokana na umbile lake la mwili na uwezo mkubwa wa kukaa na mpira miguuni pamoja na kufunga.

Wote wawili wamejiunga na Yanga katika dirisha hili kubwa la usajili linaloenda kufungwa muda mchache kutoka sasa.

Kisinda alijiunga na Yanga akitokea klabu ya AS Vita ya Congo, huku Sarpong amesajiliwa na klabu hiyo akitokea Rayon Sport ya nchini Rwanda

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!