Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaiteka nchi, mashabiki waitika
Michezo

Yanga yaiteka nchi, mashabiki waitika

Spread the love

IDADI kubwa ya mashabiki wa Yanga waliojitokeza kwenye kilele cha “Wiki ya Mwananchi” kinaweza kuwa kielelezo tosha cha kuonesha kufanikiwa kwa tamasha hilo ambalo lilijumuisha burudani za muziki kutoka kwa wasanii mbalimbali, lililofanyika Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es Salaam wenye uwezo wa kubeba watu 60,000. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)

Tamasha hilo ambalo limefanyika kwa mwaka wa pili na kuonesha mafanikio makubwa kiasi cha mashabiki kuutapisha Uwanja huku lengo kuu likiwa kuwakutanisha mashabiki wa timu hiyo pamoja na kutambulisha wachezaji watakao kwenda kutumika kwenye msimu uajo wa Ligi na mashindano mengine.

Tamasha hilo lilianza majira ya saa 4 asubuhi kwa kujumisha burudani mbalimbali kiasi cha kuvutia waliowengi kwa kufuatilia kupitia matangazo ya televisheni.

Mashabiki walijitokeza kwa wingi kuja kuona usajili mpya wa wachezaji uliofanywa na uongozi wa klabu hiyo katika siku za hivi karibuni na kufufua tena matumaini yao kwenye kulinyaka taji la Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu ujao.

Kitendo cha Yanga kuujaza uwanja huo, kimetoa jibu kwa watani zao walioshindwa kuujaza kwenye kilele cha “Simba Day.”

Huwenda likawa ni moja ya tukio lililofuatilia na idadi kubwa ya watu nje na ndani ya mipaka ya Tanzania kutokana na ukubwa wa mpira wa Tanzania ulipofikia kwa sasa.

Ukiacha uwanja kujaa  sehemu ya ndani, idadi kubwa ya mashabiki ilikuwa nje ya uwanja.

Ikumbukwe mpaka Yanga inahitimisha “Wiki ya Mwananchi” bado hawajatambulisha jezi watakazo tumia katika msimu ujao wa mashindano uliozinduliwa jana Jumapili jijini Arusha kwa mchezo wa Ngao ya Jamii uliozikutanisha Simba na Namungo na Simba kuibuka mshindi kwa 2-0.

Katika mchezo wa jana kati ya Yanga na Aigle Noir ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa 2-0 huku mchezaji aliovutia mashabiki wengi ni nyota kutoka Angola, Calinhos pamoja na Tuisila Kisinda na Tunombe Mukoko, wakitokea Congo

 

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!