CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), chini ya Mwenyekiti wake Taifa, Rais Samia Suluhu Hassan, kinatarajia kufanya vikao vyake vya kawaida jijini Dodoma, kuanzia tarehe 15 hadi 18 Desemba 2021. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa hiyo imetolewa kwa umma leo Jumanne, tarehe 14 Desemba 2021 na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Shaka Hamdu Shaka.
Taarifa ya Shaka imesema kuwa, kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), kitafanyika tarehe 18 Desemba mwaka huu, kikitanguliwa na vikao vya Kamati Kuu na Sekretarieti ya halmashauri hiyo.
“Halmashauri Kuu ya CCM itakutana Desemba 18, 2021 chini ya Mwenyekiti wetu, Rais Samia. Kikao hicho kitatanguliwa na vikao vya Kamati Kuu ya Halmashauri ya CCM Taifa na Sekretarieti ya Halmashauru Kuu ya CCM Taifa kuanzia Desemba 15, 2021,” imesema taarifa ya Shaka.
Taarifa hiyo imesema kuwa, vikao hivyo ni vya kawaida kwa mujibu wa Katiba ya CCM ya 1977 Ibara ya 108.
“Vikao vyote ni vya kawaida ambavyo vitafanyika makao makuu ya CCM jijini Dodoma, ambaoo maandalizi ya vikao hivyo yamekamilika,” imesema taarifa ya Shaka.
Leave a comment