RAIS Samia Suluhu Hassan ameipongeza Klabu ya Soka ya Simba Qeens SC kwa kutwaa ubingwa wa Afrika Mashariki wa CECAFA 2022 kwa Wanawake (SAMIA CUP). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)
Mmejenga heshima kwa soka la Tanzania na nchi kwa ujumla. Nawatakia kheri katika Ligi ya Mabingwa Afrika (2022 CAF Women’s Champions League ) itakayofanyika nchini Morocco.
Rais Samia ametoa pongezi hizo leo tarehe 28 Agosti, 2022 baada ya timu hiyo ya Simba Queens kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya She Corporates ya Uganda usiku wa jana katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la dar es Salaam.
Kupitia akaunti yake ya Twitter, Rais Samia ameandika, “Nawapongeza wanangu Simba Qeens SC kwa ubingwa wa Afrika Mashariki wa CECAFA 2022 kwa Wanawake (SAMIA CUP). Mmejenga heshima kwa soka la Tanzania na nchi kwa ujumla. Nawatakia kheri katika Ligi ya Mabingwa Afrika (2022 CAF Women’s Champions League) itakayofanyika nchini Morocco”.
Bao pekee la Simba lilitiwa kimyani na kiungo wa kimataifa wa Kenya, Vivian Corazone Aquino Odhiambo dakika ya 49 kwa penalti baada ya Asha Djafar kuangushwa kwenye boksi.
Timu hiyo ya Simba Queen itauwakilisha ukanda wa CECAFA kwenye Ligi ya mabingwa ya wanawake Oktoba mwaka huu nchini Morocco.
Pamoja na ushindi huo, Simba Queens pia wametoa kipa Bora wa mashindano, mzawa Gelwa Yona na Mchezaji Bora wa Mashindano, ambaye ni Vivian Corazone Aquino Odhiambo, huku Abela Roza wa Commercial Bank ya Ethiopia akiwa Mfungaji Bora.
Leave a comment