Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia awaachia huru mahabusu 2,240 waliobambikizwa kesi
Habari za SiasaTangulizi

Samia awaachia huru mahabusu 2,240 waliobambikizwa kesi

Spread the love

MAHABUSU zaidi ya 2,240 waliokuwa wanashikiliwa katika vyombo vya kisheria kwa kesi za kubambikizwa, wameachwa huru tangu Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, aingie madarakani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 20 Julai 2023, jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus, katika kikao cha wajumbe wa Tume ya Haki Jinai na wahariri wa vyombo vya habari, kuhusu ripoti yake iliyowasilisha kwa Rais Samia, hivi karibuni.

Zuhura amesema kuachwa huru kwa mahabusu hao, ni sehemu ya utekelezaji wa azma ya Rais Samia, kuimarisha mifumo ya haki jinai nchini.

“Kwa mfano zaidi ya mahabusu 2,240 waliokuwa wanashikiliwa kwenye vyombo mbalimbali vya kisheria wakiweko viongozi wa dini, wanasiasa na wananchi wa kawaida waliachiwa na kurejea uraiani kuendelea na maisha yao. Hii ni baada ya Rais Samia kuagiza vyombo vya utoaji haki kushughulikia masuala hayo,” amesema Zuhura.

Miongoni mwa watu mashughuli walioachwa huru kutoka mahabusu za magereza mbalimbali wakikabiliwa na mashtaka mahakamani, ni pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na walinzi wake wanne, waliokuwa wanakabiliwa na mashataka ya uhujumu uchumi.

Rais Samia Suluhu Hassan

Wengine ni baadhi ya viongozi wa dini ya kiislamu waliokuwa wanakabiliwa na mashataka ya ugaidi katika mahakama mbalimbali nchini.

Mbali na kuwaacha huru mahabusu hao, Zuhura amesema Serikali ya Rais Samia imeendelea kuimarisha mfumo wa haki jinai kwa kutekeleza masuala mbalimbali, ikiwemo kuhakikisha wananchi wanapata tafsiri za mienendo ya kesi zao kwa kutumia Kiswahili.

Pamoja na kuanzisha kampeni ya kitaifa ya utoaji huduma ya msaada wa kisheria, inayofahamika kwa jina la “Samia Legal Aid Campaign”.

Katika hatua nyingine, Zuhura amesema baada ya tume hiyo kuwasilisha ripoti yake, ameagiza taasisi zinazosimamia mfumo wa haki jinai kuyafanyia kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!