Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ripoti ya CAG yatinga bungeni
Habari za Siasa

Ripoti ya CAG yatinga bungeni

Spread the love

RIPOTI kuu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni 2023, imewasilishwa bungeni jijini Dodoma, kwa ajili ya kujadiliwa na wabunge. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Ripoti hiyo imewasilishwa leo tarehe 15 Aprili 2024, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande, ikiwa ni wiki mbili baada ya CAG Charles Kichere, kuikabidhi kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, tarehe 28 Machi mwaka huu.

Akiwasilisha hati ya ripoti hiyo mezani, Chande amesema imebeba ripoti 21 za ukaguzi, ikiwemo ripoti ya CAG kuhusu ukaguzi wa taarifa za fedha za Serikali kuu, ripoti kuhusu ukaguzi wa taarifa za fedha za mamlaka za serikali za mitaa, ripoti ya ukaguzi wa taarifa za fedha za miradi ya kimkakati na ripoti ya ukaguzi wa mashirika ya umma.

Ripoti nyingine ni ya ukaguzi wa ufanisi na ripoti ya ukaguzi wa mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

error: Content is protected !!