Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Singida atahadharisha wafanyabiashara kukopa katika taasisi zilizosajiliwa
Habari Mchanganyiko

RC Singida atahadharisha wafanyabiashara kukopa katika taasisi zilizosajiliwa

Spread the love

WAFANYABIASHARA wanaotarajia kukopa ili kuendesha biashara wameshauriwa kuchukua mikopo kwenye taasisi za kifedha ambazo zimesajiliwa na Benki Kuu (BoT). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma (endelea).

Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba alipozungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea mabanda ya maonesho ya kilimo, mifugo na uvuvi yanayofanyika kikanda katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.

Amesema taasisi zote zinazotoa mikopo zinatakiwa kuwa zimesajiliwa na Benki kuu ya Tanzania na lazima leseni za taasisi hizo ziwe sehemu ya wazi kwa nia ya mteja kujiridhisha na usajili wa taasisi husika.

Mkuu huyo wa mkoa amesema taasisi ambazo zinatoa fedha bila kuwa na usajili wa BoT zinavunja sheria ya nchi na kwa kufanya hivyo ni sawa na kuwatapeli wale ambao wamekuwa wakikopa pesa hizo kwani hawastahili kutoa mikopo hiyo.

Kwa upande wake Mwalimu wa shule ya Msingi Nzuguni, ambaye hakutaja jina lake litajwe amesema kuwa walimu wamekuwa wahanga zaidi katika mikopo umiza na wakati mwingine hulazimika kuwapatia wale wanaowakopesha kadi za benki na kila mshahara unapoingia hulazimika kukatwa pesa hizo.

Aidha, amesema kutokana na kupata elimu ya kutosha juu ya ukopaji sasa watakuwa makini katika kutambua taasisi sahihi ambazo zipo kisheria katika kukopesha badala ya kujitumbukiza katika mikopo umiza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafugaji kuku Ihemi wanufaika na mafunzo

Spread the loveWADAU  wa mnyororo wa thamani katika sekta ndogo ya kuku...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yaainisha mpango wa kusaidia wachimbaji wadogo

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameainisha mpango wa Serikali wa...

Habari Mchanganyiko

DAWASA yatekeleza agizo la Samia kwa kutangaza zabuni kielektroniki

Spread the loveKiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Godfrey Mnzava...

error: Content is protected !!