Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Ukraine acharuka, atimua bosi usalama kwa usaliti
Kimataifa

Rais Ukraine acharuka, atimua bosi usalama kwa usaliti

Spread the love

 

RAIS wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy jana tarehe 17 Julai, 2022 ametumia amri za kiutendaji kuwafuta kazi mkuu wa idara ya usalama ya wa taifa hilo – SBU pamoja na mwendesha mashtaka   mkuu nchini. Inaripoti Mitandao ya kimataifa … (endelea).

Amri ya kufukuzwa kazi kwa mkuu wa SBU, Ivan Bakanov ambaye ni rafiki wa Zelenskiyy tangu utotoni, na mwendesha mashtaka mkuu, Iryna Venediktova zilichapishwa kwenye tovuti rasmi ya rais muda mfupi baada ya hatua hiyo kuchukuliwa.

Kupitia ujumbe tofauti wa Telegram, Zelenskyy amesema kwamba amechukua hatua hiyo baada ya kubainika kwamba baadhi ya maafisa kutoka idara za wakuu hao walikuwa wakishirikiana na Russia.

Ameongeza kusema kwamba jumla ya kesi 651 za usaliti na kushirikiana na Russia zimefunguliwa dhidi ya maafisa wa usalama, huku nyingine 60 zikiwa dhidi ya maafisa kutoka ofisi za Bakankov na Benediktova.

Zelenskyy sasa ametangaza Oleksiy Symonenko kuwa mkuu mpya wa idara ya kuendesha mashitaka.

1 Comment

  • Huyu raisi anadhani vita ni mchezo. Ulaya yote iko kimya kwa sababu Urusi imeiokoa Dunia kwa kuteketeza maabara nane (8) zilizokuwa zinajaribu kutengeneza virusi kuua warusi na hata sisi waafrika.
    Wananchi sasa wamemchoka, yeye ndiyo tatizo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!