RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Polisi nchini kujipanga katika kuhakikisha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025, zinafanyika kwa amani bila kuigawa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa maafisa wakuu waandamizi wa Jeshi la Polisi, leo tarehe 4 Septemba 2023, jijini Dar es Salaam, Rais Samia amesema Serikali yake inakwenda kulitafutia fedha kiasi cha Sh. 125 bilioni, ili kuliwezesha kutekeleza majukumu yake katika kipindi hicho.
“Mwakani tuna uchaguzi wa Serikali za Mitaa, nataka jeshi liwe makini kwelikweli huko katika maeneo mbalimbali, kusimamia haki itendeke, kusimamia usalama katika chaguzi zile, kuhakikisha zinakwenda kwa njia ya usalama,”
“ IGP nimemwambia hilo akaniletea bajeti ya karibu Sh. 125 bilioni ambayo nakwenda kuipekua na ikiwezekana niipate yote ili zile changamoto ziondoke muweze kufanya kazi zenu vizuri,” amesema Rais Samia.
Rais Samia amesema ulinzi na usalama wa Tanzania unalitegemea Jeshi la Polisi “nasema kila siku Tanzania yetu ni moja tu hakuna tena Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulimwenguni, tukiweka vizuri ni sisi watanzania, tukiipasua pasua ni sisi watanzania.”
Leave a comment