Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Haya hapa mambo matatu waliyoteta Rais Samia, Dk. Ruto
Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa mambo matatu waliyoteta Rais Samia, Dk. Ruto

Spread the love

SAA chache kabla ya kuapishwa kuwa Rais wa tano wa Kenya, Dk. William Ruto ameteta na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ambaye amewasili nchini humo mapema leo kushuhudia hafla ya kuapishwa kwake. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Rais Samia Suluhu Hassan na Dk. William Ruto

Leo tarehe 13 Septemba, 2022 Dk. Ruto katika ukurasa wake wa Twitter, ameweka picha mbalimbali akiwa na Rais Samia na kuandika kuwa Serikali yake itashirikiana na Tanzania katika biashara, kilimo, usalama na maeneo mengine.

Ruto ameandika, “Tutapanua ushirikiano wetu na Tanzania katika biashara, kilimo, usalama miongoni mwa maeneo mengine yenye maslahi, mbali na kufanya kazi pamoja kwa nia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa manufaa yetu sote.”

Hata hivyo, mbali na Rais Samia, Ruto amekutana na kuzungumza na viongozi wa mataifa mbalimbali waliohudhuria sherehe ya kuapishwa kwake zinazofanyika katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!