SAA chache kabla ya kuapishwa kuwa Rais wa tano wa Kenya, Dk. William Ruto ameteta na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ambaye amewasili nchini humo mapema leo kushuhudia hafla ya kuapishwa kwake. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).
Leo tarehe 13 Septemba, 2022 Dk. Ruto katika ukurasa wake wa Twitter, ameweka picha mbalimbali akiwa na Rais Samia na kuandika kuwa Serikali yake itashirikiana na Tanzania katika biashara, kilimo, usalama na maeneo mengine.
Ruto ameandika, “Tutapanua ushirikiano wetu na Tanzania katika biashara, kilimo, usalama miongoni mwa maeneo mengine yenye maslahi, mbali na kufanya kazi pamoja kwa nia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa manufaa yetu sote.”
Hata hivyo, mbali na Rais Samia, Ruto amekutana na kuzungumza na viongozi wa mataifa mbalimbali waliohudhuria sherehe ya kuapishwa kwake zinazofanyika katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi.
Leave a comment