Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia amuahidi Ruto ushirikiano, awapongeza Wakenya kwa ukomavu kidemokrasia
Habari za SiasaTangulizi

Samia amuahidi Ruto ushirikiano, awapongeza Wakenya kwa ukomavu kidemokrasia

Spread the love

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemuahidi Rais mpya wa Tano wa Kenya, Dk. William Ruto kufanya kazi kwa kushirikiana kwa karibu katika kuleta maendeleo ya pamoja ya kijamii na kiuchumi baina ya nchi hizo na ukanda wote wa Afrika Mashariki. Anaripoti Mwandishi wetu … (endelea)

Pia amewapongeza Wakenya kwa kuonesha uikomavu wa demokrasia na kumaliza uchaguzi mkuu wa taifa hilo salama na sasa tupo wakenya na Afrika Mashariki wanashangilia uapisho wa rais huyo mpya.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo wakati akihutubia katika sherehe za uapisho wa Rais mteule Dk. William Ruto kuwa Rais wa Tano wa Kenya.

Sherehe hiyo imefanyika katika uwanja wa kimataifa wa Moi, Kasarani Nairobi.

Rais Samia mbali na kumpongeza Ruto pamoja na Naibu wake Rigathi Gachagua kwa kupokea rasmi jukumu la kuiongozi Kenya, pia amemshukuru Rais Uhuru Kenyatta kwa kumaliza vema kuitumukia nchi yake na kwa mafanikio makubwa.

“Tunawapongeza kwa kuonesha uikomavu wa demokrasia na kumaliza uchaguzi salama na leo tupo hapa pamoja kama wakenya na Afrika Mashariki tunashangilia uapisho wa rais wetu mpya.

“Nataka niwaambie kama kuna zawadi mlioitoa kwa Afrika Mashariki mwaka huu ni zawadi ya amani mliyoiweka katika uchaguzi. Tunawashukuru sana, kwa zawadi hiyo muhimu.

Amesema kwa kuwa uchaguzi umemaliza sasa wananchi wote wa Kenya washikane mikono kuijenga Kenya.

“Mwisho kama dada nitumie fursa hii kuihakikisha Kenya dhamira yetu ya dhati ya kufanya kazi kwa kushirikiana kwa karibu zaidi katika kuleta maendeleo ya pamoja ya kijamii na kiuchumi baina ya nchi zetu na ukanda wote wa Afrika Mashariki.

“Namuomba Mwenyezi Mungu amuwezeshe ndugu yetu Ruto pamoja na serikali atakayoiunda awatie nguvu ili waweze kutumikia vema nchi hii katika kiwango kinachotarajiwa na wananchi wa Kenya. Mwenyezi Mungu aibariki Kenya na Afrika Mashariki,” amemaliza Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!