Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atua K’njaro akitokea Chato
Habari za Siasa

Rais Samia atua K’njaro akitokea Chato

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Alhamis, tarehe 14 Oktoba 2021, amewasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kuanzia ziara ya siku tatu mkoani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Amewasili akitokea Chato, mkoani Kilimanjaro alikoshiriki shughuli ya kilele cha Mbio za Mwenge Maalum wa Uhuru, Kumbukizi ya miaka 22 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Wiki ya Vijana.

Mara baada ya kumaliza shughuli hiyo, aliondoka kwenda Kilimanjaro ambapo kwenye uwanja wa ndege, amepokewa na viongozi mbalimbali wa mkoa huo akiwemo Mkuu wa Mkoa, Stephen Kagaigai.

Akiwa mkoani humo, atafanya ziara na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Barabara ya Bomang’ombe-Sanya Juu-Kamwanga yenye kilomita 98.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!