Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atoa maagizo upatikanaji katiba mpya
Habari za Siasa

Rais Samia atoa maagizo upatikanaji katiba mpya

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan, ameipa maagizo Wizara ya Katiba na Sheria, ikafanyie kazi madai ya upatikanaji katiba mpya. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Agizo hilo la Rais Samia limetolewa leo tarehe 4 Aprili 2024, Ikulu jijini Dar es Salaam, akiwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni, akiwemo Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Jumanne Sagini.

Rais Samia amemtaka Sagini kushirikiana na waziri wake, Dk. Pindi Chana, kufanyia kazi suala hilo.

“Wewe (Sagini) ni mzoefu sana serikalini, utamsaidia mwenzio mambo unayoyafahamu lakini pia sasa nenda kasaidie kwenye katiba na sheria, kipindi hiki tulicho nacho watu wanadai katiba yao nenda kasaidianeni na waziri na imani yangu utaenda kufanya vizuri,” amesema Rais Samia.

Agizo hilo la Rais Samia linajiri baada ya kiongozi huyo kuwaahidi watanzania kwamba mchakato wa upatikanaji  katiba mpya utatanguliwa na zoezi la utoaji elimu ya katiba kwa wananchi katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo.

Wadau wengi hususan wa vyama vya siasa na asasi za kiraia, walipinga pendekezo hilo kwa madai kuwa linalenga kupoteza muda na kushauri mchakato huo ufufuliwe mara moja kwa kuwa kazi kubwa ilikwisha fanyika ikiwemo maandalizi ya rasimu za katiba zilizokusanya maoni kutoka kwa wananchi.

1 Comment

  • Ningekuwa na uwezo ningewaomba wale wachache wenye chama wangekubali Katiba mpya nzuri njema inayojulikana kisomi. Ee Mungu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!