Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali akiwamo Sylvester Joseph Kainda kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa iliyotolewa leo Jumatano na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus imesema kabla ya uteuzi huo, Kainda alikuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani.
Pia amemteua Eva Kiaki Nkya kuwa Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Nkya alikuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
Amemteua Chiganga Mashauri Tengwa kuwa Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Kabla ya uteuzi huu Tengwa alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Geita,
Leave a comment