RAIS Samia Suluhu Hassan, amezitaka nchi za Afrika kutumia vijana katika kuleta mageuzi ya kiuchumi barani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Mkuu huyo wa nchi, ametoa wito huo leo tarehe 26 Julai 2023 wakati akihutubia mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika kuhusu rasilimali watu, uliofanyika jijini Dar es Salaam.
“Idadi kubwa ya vijana tulionayo Afrika ni fursa ya kipekee kwa ajili ya mageuzi ya kiuchumi, badala ya kuwaacha vijana hawa wavuke hizo bahari wapigwe njiani , wazamishwe kwamba wanaenda Ulaya kutafuta maisha bora, maisha bora watayapata Afrika tukiwaendeleza,” amesema Rais Samia.
Aidha, Rais Samia amezitaka nchi za Afrika kuweka mipango madhubuti ya kuendeleza rasilimali watu kwa manufaa ya bara hilo.
Leave a comment